TATHMINI YA TAFSIRI YA JALADA LA KITABU: MIFANO KUTOKA TAFSIRI YA THE BLACK HERMIT (THIONG`O, 1968) NA KIFO KISIMANI (MBERIA, 2001)

Authors

  • Haule Jacob

Abstract

Lengo kuu la tafsiri ni kufanikisha mawasiliano kwa sababu hadhira   lengwa haijui lugha wala utamaduni chanzi. Hivyo, mfasiri anapaswa   kuwa mwaminifu kwa kulinda ukweli na ufasaha wa ujumbe wa matini   chanzi katika matini lengwa. Ujumbe huo hubebwa na vipashio   mbalimbali (maneno, virai, sentensi na aya) ambavyo mfasiri hana   budi kuvizingatia. Aidha, mfasiri huzingatia vipengele vya lugha na   masilugha vilivyomo katika jalada la tafsiri ili aweze kuandaa jalada   la matini lengwa linaloendana na ujumbe wa jalada la matini chanzi.   Hii ni kwa sababu jalada hubeba maana na ujumbe ulio kamili kwa   kutumia lugha na masilugha. Hivyo basi, makala hii imetathmini   tafsiri ya jalada la tafsiri ya tamthiliya ya The Black Hermit   iliyoandikwa na Ngugi wa Thiong`o (1968), kisha ikatafsiriwa kama   Mtawa Mweusi na Ngugi wa Thiong`o (1970) na tamthiliya ya Kifo   Kisimani iliyoandikwa na Kithaka wa Mberia (2001) na ikatafsiriwa   kama Death at the Well na Khalfan Kasu (2011). Tathmini imefanywa   kwa kuchunguza kufanana na kutofautiana kwa tafsiri za majalada   kati ya matini chanzi na matini lengwa. Makala hii imeongozwa na   Nadharia ya Usawe wa Kidhima iliyoasisiwa na Nida (1964). Data   imekusanywa kwa kutumia mbinu ya usomaji matini. Uchambuzi wa   data hiyo umetumia mbinu linganishi na mkabala wa kitaamuli.   Hatimaye, makala imebaini kuwa, licha ya vipengele kadhaa   kufanana, bado kuna tofauti zinazojitokeza katika tafsiri hizo. Jambo   hili linasababisha kutowiana kwa baadhi ya maudhui ya MC na ML.   Hivyo, makala inapendekeza kwamba si kila jalada lazima litafsiriwe.   Kutafsiriwa ama kutotafsiriwa kwa jalada la kitabu kunategemea   muktadha wa tafsiri husika.

Downloads

Published

2021-10-05

How to Cite

Jacob, H. (2021). TATHMINI YA TAFSIRI YA JALADA LA KITABU: MIFANO KUTOKA TAFSIRI YA THE BLACK HERMIT (THIONG`O, 1968) NA KIFO KISIMANI (MBERIA, 2001). JARIDA LA MNYAMPALA, 2(1), 1–13. Retrieved from https://journals.sjut.ac.tz/index.php/mnyampala/article/view/7

Issue

Section

ARTICLES