ATHARI ZA MFUMO WA VIHUSISHI VYA KINANDI KATIKA UAMILIAJI WA KISWAHILI KAMA L2 MIONGONI MWA WANAFUNZI WANAOSEMA KINANDI KAMA L1

Authors

  • Susan Chebet-Choge

Abstract

Uamiliaji wa L2 ni tukio lisiloepukika katika karne ya sasa yenye migusano mingi  ya lugha inayosababishwa na mitagusano ya watu wanaosema lugha tofauti na  kupitia ujifunzaji na ubwiaji wa lugha. Uamiliaji wa L2 ni zao la maendeleo ya  binadamu, kijamii, kiuchumi na kisiasa. Maendeleo haya hulazimisha nchi na watu  kujifunza lugha nyingine ili mahitaji fulani ya maendeleo yaweze kuafikiwa.  Uamilijia huu unakuwa wa lazima ili watu wanaosema lugha tofauti waweze  kuelewana na kubadilishana mawazo. Mwamiliaji wa L2 mara nyingi hukumbwa na  changamoto ya kuathiriwa na mfumo wa kiisimu wa LI. Athari kutoka L1 ni za  kifonetiki, kifonolojia, kimofolojia, kisintaksia na kisemantiki, ambazo  zinamwaathiri mwamiliaji wa L2. Makala hii imeshughulikia athari za  kimofosintaksia za mfumo wa vihusishi vya Kinandi katika insha za Kiswahili za  wanafunzi wanaosema Kinandi kama L1. Ni zao la utafiti uliofanywa katika shule  tatu za msingi katika Kaunti ya Nandi nchini Kenya kwa minajili ya kuandaa tasnifu  ya uzamili. Katika utafiti huo, shule hizi zilirejelewa kwa akronimu NSB. Utafiti huo  ulibainisha changamoto nyingi za kiisimu-nafsia katika kiwango cha  kimofosintaksia zinazomkumba mwanafunzi anayesema Kinandi kama L1  anapoamilia Kiswahili kama L2. Mojawapo ya vyanzo vya changamoto hizi ni  athari za mfumo wa vihusishi vya Kinandi zinazojadiliwa katika makala hii.

Downloads

Published

2021-10-05

How to Cite

Chebet-Choge, S. (2021). ATHARI ZA MFUMO WA VIHUSISHI VYA KINANDI KATIKA UAMILIAJI WA KISWAHILI KAMA L2 MIONGONI MWA WANAFUNZI WANAOSEMA KINANDI KAMA L1. JARIDA LA MNYAMPALA, 2(1), 120–133. Retrieved from https://journals.sjut.ac.tz/index.php/mnyampala/article/view/6

Issue

Section

ARTICLES