MAUDHUI KATIKA NYIMBO ZA TOHARA ZA WAMASAABA NCHINI UGANDA

Authors

  • Wanyenya Willy

Abstract

Makala hii inaeleza maudhui mbalimbali yanayopatikana katika nyimbo za tohara za Wamasaaba nchini Uganda. Kulingana na   wataalamu mbalimbali wa fasihi, maudhui ni mambo muhimu yanayopatikana katika kazi za sanaa. Nyimbo za tohara ni miongoni mwa kazi za sanaa ambazo hutekelezwa na binadamu. Katika makala   hii, mwandishi anazingatia nadharia ya ethnografia na utendaji   ambayo inalenga watu na ubunifu wao. Kwa kuzingatia nadharia hii, mwandishi anaeleza jinsi wanasanaa mbalimbali wanavyobuni   nyimbo ili kuwasilisha mawazo yao. Mwandishi anafanya hivyo kwa   kurejelea angalau mfano mmoja wa nyimbo hizo kwa kila maudhui. Mwandishi amepanga maudhui hayo kulingana na utaratibu wa   utendaji wa nyimbo hizo za tohara. Kutokana na jambo hili, mwandishi anaangalia mambo mbalimbali katika utekelezaji wa tohara kwa sababu nyimbo hizo huambatana na matendo fulani. Hapa, mwandishi ametaja tendo linalotekelezwa na kutoa mfano wa   wimbo unaoimbwa. Baada ya kutoa mfano wa wimbo,   anauchanganua na kubainisha maudhui yaliyomo. Maudhui   yanayowasilishwa yanaonesha mchakato mzima wa utendaji wa   tohara kuanzia siku ya kwanza hadi ya tatu, wakati ambapo utendaji wa tohara yenyewe hukamilika. Nyimbo ambazo zimenukuliwa   zinaonesha mambo kama vile: matayarisho ya tohara, vijana kuzuru ugenini, vijana kuondoka ugenini, vijana kujipa hamasa, na vijana kuondolea jamaa zao wasiwasi.

Downloads

Published

2021-10-05

How to Cite

Willy, W. (2021). MAUDHUI KATIKA NYIMBO ZA TOHARA ZA WAMASAABA NCHINI UGANDA. JARIDA LA MNYAMPALA, 2(1), 14–31. Retrieved from https://journals.sjut.ac.tz/index.php/mnyampala/article/view/13

Issue

Section

ARTICLES