UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI WA MOFOLOJIA PAMOJA NA UMILISI WA KIWANGO CHA CHINI MIONGONI MWA WANAFUNZI WA VYUO VIKUU NCHINI UGANDA

Authors

  • Mulei Martin

Abstract

Ufundishaji na ujifunzaji wa masomo ya isimu katika lugha ya   Kiswahili vyuoni umeathiriwa na changamoto kadhaa. Miongoni   mwazo ni matumizi ya misamiati ya kisayansi ambayo imeathiri   upataji na ukuaji wa umilisi wa taaluma za kiisimu. Makala hii   inalenga kufafanua dhana muhimu katika uchunguzi na uchambuzi wa   mofolojia, kuonesha changamoto za ujifunzaji na ufundishaji wake, na   kutoa mapendekezo ya kuondokana na changamoto hizo kwa   wanafunzi wa vyuo vikuu nchini Uganda na kwingineko. Data   ilikusanywa kupitia kwa mijadala shirikishi na usaili kutoka kwa   wanafunzi 70 na walimu 9 wa isimu walioteuliwa kimaksudi kutoka   katika vyuo vikuu vitatu nchini Uganda. Matokeo yaliyoelezwa kwa   muundo wa kimaelezo yalidhihirisha changamoto za kiisimu na zisizo   za kiisimu zilizoathiri upataji wa umilisi wa somo la mofolojia. Nazo   ni pamoja na: umilisi wa chini katika matumizi ya Kiswahili sanifu,   ugumu na kukanganywa katika kueleza dhana za kimofolojia,   mitazamo hasi, pamoja na uchache wa vitabu vya isimu vinavyokidhi   masilahi ya wanafunzi wa viwango vyote vya umilisi. Utafiti   ulipendekeza kuwapo kwa mijadala na makongamano, uandishi wa   vitabu mwafaka vya isimu, na kujenga uchanya wa ujifunzaji wa somo   la mofolojia.

Downloads

Published

2021-10-05

How to Cite

Martin, M. (2021). UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI WA MOFOLOJIA PAMOJA NA UMILISI WA KIWANGO CHA CHINI MIONGONI MWA WANAFUNZI WA VYUO VIKUU NCHINI UGANDA. JARIDA LA MNYAMPALA, 2(1), 47–64. Retrieved from https://journals.sjut.ac.tz/index.php/mnyampala/article/view/10

Issue

Section

ARTICLES